Rais Samia Suluhu awateua wakuu wapya wa mikoa Tanzania, huku baadhi wakistaafu
Rais Samia Suluhu awateua wakuu wapya wa mikoa Tanzania, huku baadhi wakistaafu

CHANZO CHA PICHA,SAMIA SULUHU/TWITTER
Katika mabadiliko aliyoyafanya kwa wakuu wa mikoa Tanzania kuna sura ngeni katika ngazi hii ya uongoz
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan leo amefanya mabadiliko ya Wakuu wa mikoa, huku wengi wao wakihamishiwa katika mikoa mipya na wengine wakistaafu utumishi wa umma.
Taarifa ya uteuzi wa wakuu hao wa taasisi pamoja na wakuu wa mikoa ulioanza leo Jumamosi Mei 15, 2021 imetolewa leo na mkurugenzi wa mawasiliano ya rais Ikulu, Gerson Msigwa, ikieleza kuwa wataapishwa Mei 18, 2021 Ikulu, jijini Dar es Salaam.
Hatahivyo, Rais Samia ameingiza sura chache mpya katika ngazi hiyo ya utawala, akiwemo aliyekuwa mgombea wa kiti cha urais kutoka upinzani Queen Sendiga na Amos Makalla ambaye anarejea tena uongozini baada ya miaka mingi.
Wengi miongoni mwa wale walioachwa nje ya orodha ndefu ya watu 45 ni 10 na wanasemekana kuwa wamefikisha umri wa kustaafu, na wanajumuisha mwanamke mmoja kutoka upinzani mama Mgwira.
Maoni